NAIBU WAZIRI MH.BITEKO AIPONGEZA BoT KWA KUANZA KUNUNUA DHAHABU
NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Maonesho ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini, mkoani Geita na kuipongeza BoT kwa kuanza kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji na wauzaji wa dhahabu nchini kwa lengo la kuongeza akiba ya fedha za kigeni.
Aidha, Dkt. Biteko ameitaka BoT kushirikiana na Wizara ya Madini katika utekelezaji wa zoezi hili litakalochangia maendeleo ya sekta ya madini na ustawi wa uchumi wetu.



Comments
Post a Comment