VETA WASHIRIKI MAONESHO YA TISA YA SAYANSI ,TEKNOLOJIA NA UBUNIFU
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM
CHUO cha Ufundi Stadi VETA Dar es Salaam wameshiriki kwenye Kongamano la tisa la Maonesho ya Sayansi,Teknolojia na Ubunifu linalofanyika Jijini Dar es Salaam ambapo kwa kipindi cha miaka mitano wamefanikiwa kuibua bunifu 118 na kati ya hizo 13 zimeingizwa sokoni na 45 zipo katika mchakato wa kuingizwa sokoni.
Meneja Uhusiano kwa Umma Veta, Sitta Peter, ameyasema hayo leo, Desemba 2, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Kongamano la hilo.
Meneja Peter amesema kwamba katika bunifu hizo zipo dawa mbalimbali kama dawa za UTI, fangasi na za kuzuia mbu waenezao malaria .
Pia amefafanuana kuwaomba Watanzania kutumia dawa hizo ili kuwaongezea hamasa za kuendelea kubuni dawa nyingine zitakazokidhi mahitaji kwa wananchi.
"Maonesho haya ni moja ya kazi zetu na sehemu ya kuwaonesha watanzania na jamii kwa ujumla ambavyo tumeweza kufanikiwa katika kufundisha na kubuni bidhaa mbalimbali ambazo zinaweza kuwa msaada kwa jamii"amesema
Mwalimu wa Chuo Cha VETA Dar es Salaam Ally Issa amesema kutokana na kufanikiwa kubuni bidhaa mbalimbali na tayari wamezipatia hati miliki ili bunifu hizo zisiweze kuchukuliwa au kuigwa na wengine.
Mwalimu Issa ameendelea kwa kusema kwamba bidhaa ambazo bado hatujaziingiza sokoni tunaendelea na mchakato wa kupata miliki bunifu na tunatumaini kwamba tutafanikiwa.
Kwa upande wake Mvumbuzi wa kifaa cha kufundushia mfumo wa jua na muundo wa Atomu, Ernest Maranya amesema tayari kifaa hicho kimepata ruhusa ya kufundishia kwenye shule za msingi na sekondari baada ya kupata Ithibaki kutoka Wizara ya Elimu.
Mvumbuzi Maranya ameiomba Serikali na wadau wa elimu kumsaidia mtaji ili aweze kutengeza kifaa hicho kwa wingi jambo litakalosaidia kufikia malengo ya kutawanywa kwenye shule mbalimbali nchini.
"Kupitia kifaa hiki ninaamini wanafunzi wengi wataweza kuelewa vizuri somo la mifumo ya jua, hivyo naomba wadau wa elimu wanisaidie mtaji ili niweze kutengeneza kifaa hiki kwa wingi na kiweze kuwafikia wanafunzi wengi na kwa wakati",amesema



Comments
Post a Comment