PURA YATOA WITO KWA WAWEKEZAJI KUWEKEZA KATIKA NISHATI SAFI
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline
Dar es Salaam
MKURUGENZI wa Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA),Mhandisi Charles Sangweni ametoa wito kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika Nishati Safi kutokana na kuwepo mikakati imara yenye mazingira wezeshi, amani na utulivu inayotoa fursa kwa maendeleo ya kiuchumi.
Pia Sangwenin amesema kwamba kutokana na kuwepo kwa mazingira wezeshi, amani na utulivu shughuli za uzalishaji katika mkondo wa Juu wa Petrol kwenye nyanja ya ajira imeongezeka kutoka asilimia 55 hadi 85.
Hayo ameyabainisha leo julai 9 katika Viwanja vya sabasaba ambapo Maonesho ya 49 ya kimataifa yanaendelea wakati akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kutembelea na kujionea hali halisi ya Maonesho hayo.



Comments
Post a Comment