TBA KUSHIRIKISHA SEKTA BINAFSI KWENYE MIRADI
Na Mwandishi wetu,MwelekeoMedia. Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imepanga kushirikisha sekta binafsi katika miradi yao ili kusaidia kuondoa changamoto ya nyumba kwa watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla Akizungumza leo jijini Dar es Salaam octoba 16, baada ya kutembelea miradi mitatu ya TBA, Mkurugenzi wa Idara ya Miliki TBA, Said Mndeme amesema kuwa mahitaji ya nyumba yamekuwa yakiongezeka kila mwaka. "Machi mwaka jana Rais Dk.Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa nyumba za Magomeni Kota, alitutaka TBA na taasisi nyingine za Serikali zinazioshughulikia ujenzi wa makazi ya watu kushirikiana na sekta binafsi za nje au ndani kwani Kwa kufanya hivyo zitaweza kuendeleza makazi bora kwa haraka kuliko kusubiri Serikali kukusanya fedha ambazo haziwezi kukidhi uhitaji wa haraka wa makazi hayo, " amesema. Amesema agizo hilo la Rais Dk. Samia liliungwa mkono na wabunge ambao waliishauri TBA, kushirikiana na sekta binafsi ili kuongeza uwezo wa kujenga ny...