Posts

Showing posts from September, 2023

MAVUNDE AIPONGEZA KAMPUNI YA BLUE COAST KWA UTENDAJI WAKE ULIOTUKUKA

Image
Na Prosper Rutayuga,MwelekeoMedia  Serikali imesema itaendelea kusimamia sheria ya Local contect ili kuhakikisha watanzania wananufaika na rasilimali zao ikiwemo madini ya dhahabu . Hayo yamesemwa na Waziri wa Madini  Antony Mavunde alipomtembelea mmoja wa wawekezaji wazawa mkoani Geita ,Athanas Inyasi  anaemiliki kampuni ya blue coast  ili kujionea namna alivyonufaika  na sheria ya Local contect ambapo amewasisitiza wafanyabiashara ,wachimbaji kujitokeza kuomba zabuni . "Nitoe rai kwa makampuni mengine yakitanzania kuchangamkia fursa hii sisi kama tutahakikisha tunaisimamia sheia hii vizuri ili watanzania wengi  zaidi waweze kunufaika tunahitaji kuwaona  akina mzee Inyasi wengi zaidi kama alivyomsema mkuu wa Mkoa ili mwisho wa siku tuweze kuyaona matokeo ya uchumi wa madini  katika maisha ya watanzania na kupitia uchumi huu tuweze kukuza pia uchumi wa tanzania na jambo hili linawezekana",amesema Mavunde. Aidha Waziri Mavunde amesema kuwa...

MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI YATOA ELIMU YA UTAMBUZI WA BIDHAA ZILIZO CHINI YA KIWANGO

Image
Na Prosper Rutayuga,MwelekeoMedia  Sabanitho Mtega ambaye ni Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Bidhaa na Mazingira kutoka Mamlaka ya Maabara na Mkemia Mkuu wa Serikali  amewataka Wachimbaji wadogo kuhakikisha wanatumia vifaa kwa ajili ya kujikinga ili kuepuka na madhara yatokanayo na kemikali  wanazotumia wakati wa utafutaji wa madini. Mwito huo  ametoa Septemba 27 mwaka huu  wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini chini ya kauli mbiu " Matumizi ya Teknolojia sahihi katika kuinua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuhifadhi Mazingira"  yanayofanyika katika viwanja vya EPZA Bombambili mkoani Geita. Mtega amesema  tatizo kubwa linalowakabili wachimbaji wadogo wa Madini  ni kutumia kemikali bila kuvaa vifaa vya kuzuia ama  kujilinda afya zao,hali inayowapelekea baadaye  kupata madhara ya kiafya. " Kwenye tasnia ya Madini,  kwenye utafutaji wanatumia kemikali, kwenye uchimbaji pia hivy...

ZAIDI YA BILIONI 5 YATUMIKA UWEKEZAJI WA MAABARA YA KISASA YA UPIMAJI WA SAMPULI ZA MADINI, MSALABS GEITA

Image
Na Prosper Rutayuga, MwelekeoMedia  Kampuni ya MSALABS yatumia zaidi ya Shilingi za kitanzani Bilioni 5 katika uwekezaji wa Maabara ya kisasa inayopima sampuli za Madini kwa kiwango cha kimataifa mkoani Geita. Hayo yamebainishwa Septemba 27, 2023 na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Maabara ya MSA Mugisha Lwekoramu wakati wa ufunguzi wa Maabara hiyo iliyoanzishwa mwaka 2020 ikiwa ni kampuni tanzu ya MSALABS yenye makao makuu yake nchini Canada Akizungumzia kuhusu teknolojia inayotumika katika Maabara hiyo Lweramu amesema Maabara hii inatumia teknolojia ya kisasa ya upimaji wa sampuli kwa mionzi yaani (PhotoAssay) ambayo ni rafiki kwa utunzaji mazingira kwasababu haitumii kemikali au moto katika upimaji sampuli. Akielezea kuhusu ufanisi wa teknolojia hiyo amesema hii ni sehemu ya mapinduzi ya teknolojia kwasababu inamwezesha mdau kupata majibu ya sampuli ndani ya masaa mawili ni tofauti ukilinganisha na teknolojia ya zamani ya kutumia moto na kemikali. Kwa upande Waziri wa Madini An...

SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KATIKA KUENDELEZA MILKI NCHINI

Image
Na Mwandishi Wetu, MwelekeoMedia  Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kupitia vifungu vyake imeona haja ya kushirikiana na Sekta binafsi ili kuendeleza miliki  nchini. Hayo yamebainishwa Jana na Kaimu Meneja Mawasiliano na Masoko  Wakala wa Majengo Tanzania (TBA ) Fredrick Kalinga mbele ya Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Constantine Kanyasu alipokua akitembelea mabanda ya Maonyesho ya sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini chini ya kauli mbiu " Matumizi ya Teknolojia sahihi katika kuinua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuhifadhi Mazingira"  yanayofanyika katika viwanja vya EPZA Bombambili Halmashauri ya Mji Geita. Kalinga amesema Serikali ya awamu ya sita kwa kuona haja ya kuhuisha Sheria iliyoanzisha Wakala wa Majengo Tanzania ( TBA ) kwa kuiboresha kupitia GN namba 595  Agosti 25, 2023 ambayo inairuhusu TBA kushirikiana na Sekta Binafsi kuendeleza miliki nchini (kujenga nyumba za kupangisha na kuuza kwa wananchi wote) " Tunaishukuru Ser...

MBUNGE KANYASU AWAPONGEZA WAANDAAJI WA MAONESHO YA 6 YA TEKNOLOJIA YA MADINI

Image
Na Mwandishi Wetu,MwelekeoMedia  Mh. Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini amewapongeza waandaaji wa Maonyesho ya 6 ya kimataifa ya Teknolojia ya madini na pia kupata nafasi ya kuwa Mgeni mahususi katika kutembelea mabanda mbalimbali yaliyoko katika Maonyesho hayo Ambapo amesema Maonyesho yameandaliwa vizuri na washiriki ni wengi hivo inatia hamasa, hususani ushiriki wa bidhaa mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi umeongezeka,  pia kuongezewa Kwa makampuni ya Madini hasa wanaonyesha Teknolojia ya Madini. Kanyasu amesema Kwa mara ya kwanza Maonyesho hayo yameleta Watanzania wanaochimba Madini kutoka Mikoa nanhata nje ya nchi  kuja kutangaza Biashara zao Tanzania, hivyo amewapongeza waandaaji Kwa jambo hilo kubwa na muhimu. " Lakini pia kwa mara ya kwanza Maonyesho hayo yameleta Watanzania wanaochimba Madini kutoka Mikoa mbalimbali  na hata nje ya nchi kuja Tanzania kutangaza biashara zao, hivyo niwapongeze sana wandaaji Kwa jambo hili kumbwa na muh...

TIRA YAWAASA WANANCHI KUTUMIA BIMA KWA MANUFAA YAO NA TAIFA KWA UJUMLA

Image
Na Mwandishi Wetu, MwelekeoMedia  MENEJA wa TIRA Kanda ya ziwa Richard Toyota Amesema kuwa Kwa ajili ya kuwapa elimu ya Bima wananchi hususani wa Kanda ya ziwa hivi Sasa wapo kwenye viwanja vya maonyesho vya EPZA Bombali mkoani Geita. Amesema kuwa wamejipanga kutoa elimu kwa watanzania wote wakiwamo wachimbaji wadogo ,wakubwa na wawekezaji ,wakulima ,wafugaji,wavuvi na watu wa Kila aina ambao watakuwa wamefika kwenye viwanja hivyo. Toyota ameyasema haya Septemba 26 mwaka huu kwenye viwanja hivyo vya maonyesho ya Teknolojia ya madini katika mahojiano yake na waandishi wa Habari waliotaka kujua ushiriki wao katika maonyesho hayo. Meneja Toyota Amesema kuwa kwakuwa Bima  ni ulinzi au Kinga Kwa mana hiyo Kila mtu anahitaji Ulinzi nakkwamba kwakuwa Kila mmoja anaasiliwa na majamba mbalimbali ya kiuchimi basi anahitaji kuwa na Bima . Amefafanua kuwa jambo la msingi la kujiuliza ni kwamba wewe unahitaji  Bima ya aina gani na kwamba misingi gani Kwa mafano wawekezaji wadogo wanab...

RITA - WANANCHI KUWENI NA DESTURI YA KUANDIKA WOSIA ILI KUONDOA MIGOGORO

Image
Na Mwandishi wetu, Mwelekeomedia  WAKALA Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) umewataka wananchi Kujenga desturi ya kuandika wosia Ili kuondoa migogoro ya mirathi inayochukua muda mwingi kufuatilia kes mahakamani badala ya muda huo kuutumia kwenye shughuli za uzalishaji Mali. Hayo yamesemwa na Wakili wa Serikali kutoka RITA  Rwegasira wakati akizungumza na waandishi wa Habari kwenye maonesho ya sita ya Kimataifa na Teknolojia 2023 mkoani Geita.  "Sisi tuna kaulimbi inasema 'kuandika wosia siyo uchuro'ikiwa na maana kwamba kuandika wosia ni utaratibu  ambao binadamu anatakiwa awe nao ili kujua siku asipokiwepo mali zake zinagawanywa katika utaratibu bila kuleta migogoro."amesema Rwegasira na kuongeza kuwa   "Tunashuhudia katika vyombo vya habari watu wanagombania Mali alizoacha marejemu lakini kumbe angekuwa ameacha waraka kwamba Mali zinagawanywaje migogoro kwenye jamii isingekuwepo na watu wasingetumia muda miwngi kugombana  kwa kwenda mahaka...

BODI YA NAFAKA YADHAMIRIA KUMUONDOLEA MKULIMA CHANGAMOTO ZA SOKO

Image
Francisco Amos,ambae ni   Afisa masoko na usambazaji kutoka Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko (PCB)    amesema kuwa bodi imejipanga kumuondolea mkulima changamoto ya soko ya mazao yao iliyokuwa inamkabili mkulima huko nyuma  Akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya sita ya teknolojia ya madini yanayofanyika katika viwanja vya EPZA Bobambili mkoani Geita,Amos amesema kuwa Serikali ilianzisha bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko ili iwe jukwaa la wakulima kuuza mazao yao pindi wanapopata changamoto katika masoko au mavuno yao.  "Naweza kusema kwamba tumeshiriki maonyeaho haya tukiwa na lengo la kuonyesha bidhaa bora zinazozalishwa na bodi hiyo kupitia viwanda vyake mbalimbali hapa nchini pamoja na kuwafahamisha fursa mbalimbali ambazo bodi ya nafaka wanazitoa kwa wakazi wa Geita ikiwemo kuuza mazao yao katika bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko huduma za uwakala usambazaji na vilevile tunatoa ushauri wa kitalaamu wa maswala ya...

MIKAKATI YA REA KATIKA KUHAKIKISHA VIJIJI VYOTE TZ VINAPATA UMEME

Image
Na Prosper Rutayuga, MwelekeoMedia SERIKALI kupitia Wakala  wa Nishati vijijini (REA) umefanikiwa kufikisha  nishati ya umeme vijijini katika vijiji 10,987 ambayo karibu asilimia 89 ya vijiji vyote  12318 vilivyopo hapa nchini vimeshafikiwa na umeme.tu ambavyo baadhi yake wakandarasi wapo saiti wanaendelea na kazi. Amesema matarajio mpaka mwakani vijiji vyote vitakuwa vimeshafikiwa na umeme lakini vijiji vingi  vitapata umeme kabla ya desemba mwaka huu na vingine mwakani. “Kwa hiyo tukimaliza zoezi la kupeleka umeme vijijini tunahamia kwenye vitongoji ingawa mradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji tulikuwa tumeshauanza .”amesema  Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo ,Tanzania Bara ina vitongoji 64,760 ambapo karibu vitongoji 28586 vimeshafikiwa na umeme kwa hiyo utakuja kuona kuna vitoingoji 36,000 ndio bado havijafikiwa na umeme.  “Kama mnavyofahamu Tanzania tumebarikiwa nchi yetu ni kubwa ,Tanzania peke yake ukijumlisha Kenya, Uganda , Ruanda na Burundi yaani A...

FCC YATETA NA WADAU WA SEKTA YA MADINI GEITA

Image
Na Mwandishi wetu, MwelekeoMedia  Ndg. Mgasi Kalindimya,ambae ni mkaguzi wa bidhaa bandia wa Tume ya Ushindani (FCC) amesema wameshiriki katika Maonyesho ya sita ya madini kwa lengo la kutaka kumfikia mtumiaji na mlaji wa bidhaa ambaye anapokea huduma moja kwa moja kutoka Kwa wadhalishaji. Amesema kuwa wapo kwaajili ya kuangalia watu mbalimbali ambao wanachukua mikopo ya wajasiliamali wadogo wadogo ili kuwasaidia kuwapa elimu ya namna bora ya kutumia mikopo hiyo katika masuala ya teknolojia. Ameyasema hayo Septemba 24, 2023 AFISA mkaguzi bidhaa bandia wa Tume ya Ushindani (FCC) Mgasi Kalindimya katika viwanja vya maonyesho ya sita ya teknolojia ya madini, yanayoendelea mkoani Geita. Amesema FCC ni Taasisi ya Serikali ambayo ipo chini ya Wizara ya Viwanda na biashara na inasimamia sheria mbili ambazo watu wanaokuja kwenye maonyesho wanapaswa kutambua hilo.  "Tunasheria mbili ambazo tunazisimamia sokoni, tunasheria ya alama za bidhaa ambayo hii inatupa nguvu ya kupambana na bidh...

WAZIRI MAVUNDE AIPA TANO GF TRUCKS KWA KUWAPATIA VIFAA WACHIMBAJI MADINI KWA NJIA RAHISI

Image
Na Prosper Rutayuga, MwelekeoMedia  Kampuni ya GF Trucks&Equipment inayojishughulisha na uuzaji wa magari,mashine na mitambo kwa ajili ya shughuli mbalimbali zikiwemo za uchimbaji Madini leo umepokea kongole kutoka kwa waziri  wa Madini Anthony Mavunde  kwa kuona umuhimu wa kushirikiana na sekta ya madini hasa wachimbaji katika kuwapatia vifaa katika mfumo ambao utawezesha wachimbaji wengi kumiliki vifaa vitakavyosaidia katika shughuli za uchimbaji. Akizungumza katika uzinduzi wa Ofisi ya GF Truck mkoani Geita,Mavunde amewaomba waendelee kutanua wigo na kuwezesha wachambiji wengi zaidi kupata vifaa hivyo ambavyo vitaleta tija kubwa katika Taifa. “Na sisi kama Wizara ,kwa kuwa tunao mkakati wa kuhakikisha kwamba tunaongeza shuguli za uzalishaji wa madini hapa nchini wa kuongeza wigo mpana zaidi wa madini ya aina mbalimbali kwa tafiti ambazo tutakwenda kuzifanya .”amesema Mavunde Aidha ametumia nafasi  hiyo kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Madini n...

NGUVU MOJA SECURITY MKOMBOZI WA WADAU WA MADINI KATIKA SEKTA YA ULINZI

Image
Na Prosper Rutayuga, MwelekeoMedia KAMPUNI ya Nguvu Moja ( Security services limited ) inayoshughulikia ulinzi ni Moja ya Kampuni inayoshughulikia suala la ulinzi sehemu mbali mbali imekua ikilinda afya ikijali afya ya wafanyakazi pamoja Mazingira wanayoishi pamoja na magonjwa. Hayo yamebainishwa septemba 23 mwaka huu na Meneja wa Kampuni ya Nguvu Moja Services limited Caroline Mushi ambapo amesema kampuni hiyo imekua na tabia ya kuwapima afya wafanyakazi wake kabla ya kuingia kazini, na Mwaka mmoja akiwa kazini. " Tunapoajiri wafanyakazi wetu, kitu cha kwanza sisi hatutaki mfanyakazi anayeugua ugua kazini, kwahiyo tunampima kabla hajaingia kazini, pia tutampima afya yake baada ya Mwaka mmoja akiwa kazini, vile vile ikitokea mfanyakazi akasema hawezi kuendelea na kazi na Nguvu Moja Security services au mkataba umekwisha, au amesema ameenda kusoma, pia tutampima afya yake. "Tunampima kwa sababu gani tunataka tuhakikishe mfanyakazi tulivyompokea ana afya bora, anaweza ku...